Monday, 8 July 2013


                                           
           BLIND GIRL’S LOVE (PENZI LA MSICHANA KIPOFU)

        Neno penzi kila mmoja analichukulia kwa uzito wake na kwa namna na huwa haliingiliwi na mtu mtu zaidi ya wapendanao.
kutana na kijana Imma aliyejikuta kwenye penzi la binti kipofu (Salma) mrembo mwenye umbo la kuvutia na sauti iliyolaini yenye kubembeleza ambaye hayuko tayari kusikia neon Mapenzi kwenye maisha yake  kutoka kwenye familia kimasikini, huku wazazi wake imma wakimpinga kipofu huyu kwa kudai kuwa na mahusisano na kipofu ni mkosi kwenye familia hasa ya kitajiri kama yake.
Huku wakimlazimisha kuwa na uhusiana na Rose binti kutoka kwa mzee Martini Tajiri maarufu mkoani Tanga.
   Mmmmmhhhh nini ktatokea?
 Je Imma anaweza kupangiwa mtu wa kuwa nae na hata akiwa na Salma wakati wazazi hawako radhi, maisha yao yatakuwaje?
 Fuatilia hadithi hii tamu yenye kufunza na kusisimua kuazia sehemu kwanza hadi ya mwisho kila wiki kutoka Kwa mtunzi wako MR.Njama.

                                     SEHEMU YA KWANZA
Ni asubuhi Mwanana ndani ya jiji la tanga nyumbani kwa kina Imma Salimu mlango unagongwa na mlinzi anafungua. Ulikuwa ni msafara wa magari yasiyopungua matano na wageni wanaingia ndani ya jumba la kifahari la mzee Mwanjala liiloko barabara ya irishihni na moja katika jiji la Tanga nchini Tanzania, mara baada ya salaam Mzee mmoja anaonekeana kuongea kwa sauti ya chini na Mzee Mwanjala kasha mzee Mwanjala anaamuru Imma aitwe.
 je ni wakina nani na wanashida gani  na Imma? endelea………………

Ulikuwa msafara wa Mzee Martini ambae alikuwa mfanyakazi wa bandari ya tanga na baada ya kustaafu  anapewa pensheni yake,ni Mzee wa makamo kidogo  mwenye mtoto mmoja tu wakike aitwae  Rose.

Imma anaamka na kukuta watu wamejaa kwao pembeni anamuona msichana mrembo  anaemfahamu si mwengine bali ni Rose Martini.
Imma ni kijana mwenye umri wa miaka ishirinina na mbili aliyepata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Future Light  iliyomo tarafa ya Maramba  mkoani Tanga  na kufanikiwa kwenda Sekondari Mkwakwani ambako alipata elimu yake hadi kidato cha sita  na kufanikiwa kwenda chuo che elimu ya biashara (cbe) kilichoko jijini dar es slaam baada ya kupata Degree yake ya kwanza ya biashara anapelekwa nje ya nchi kuchukua Digrii ya pili nchini Canada akiwa huko anakutana na Muafrika mwenzie sio mwengine bali ni msichana Rose Martini kama ilivyo kawaidia kwa uatamaduni wa wa Afrika wakutanappo nje huwa kama ndugu lakini hwa ilikuwa tofauti kwani kilammoja alionekana kutomjali mwenzanke ingawa Imma alitamani sana wafahamiane
 Baada ya kuchuniana kwa muda wa wiki mbili tangu Rose na Imma wakutane kwenye chumba cha kulia chakula. ingawa Imma alionyesha kumjali Rose Lakini Rose alizidi kujiona kama hata hahisi kama Imma ni mwa afrika mwenzie kwani alikuwa busy muda wote na marafiki wa kizungu na kumuona Imma kama mluga luga Fulani baada ya wiki mbili kuisha Imma akiwa kwenye bustani ya kupumzika hii ni baada ya kuchoshwa na masomo kwa mbali anamuona msichana huyo mrembo Rose anakuja huku akiwa na bia mbili mkononi.
Hi bro? aanza kwa kumsalimia Imma
Hi how are you? anajibu Imma.
Am doing fine are you from Africa? anauliza Rose
Yes iam    anamjibu Imma.
wow which country please? anaendelea kuuliza Rose huku akiwa anakaa kwenye bustani hiyo akiwa na kisket kifupi huku nguo ya ndani ikiwa nje huku akiamini kabisa Imma atakuwa anaiona.
Tanzania, are you from Nigeria? anajibu Imma huku akisukumizia na swali.
 No you can not be serious are real Tanzanian? That my country am also from there anajibu Rose huku akionesha kutoamini kwa dhati kuwa Imma ni Mtanzania mwenzake.
 can you speak Swahili? anauliza Rose.
 yes I can anajibu Imma kwa kujiamini.
ok lets make it anamalizia Rose kwa kumuomba sasa waongee kinyumbani.
  Mbona uko peke yako hapa bustanini? aliuliza Rose.
Yaa huwa napenda kukaa peke yangu ingawa pia sina kampani, alijibu Imaa kwa style ya kuchombeza huku jicho lake likiwa kwenye mwili wa Rose mmmhhhh.
Mhhhhh huna kampani au huzitaki’’ kabla Imma hajajibu anadakia tena Rse ‘’
   Unakumbuka ,mara ya kwanza tulipoonana nilitamani sana kuwa karibu na wewe ila nikagundua uko Serious sana. ‘’hapana mbona wewe ndio ulionyesha kuwa Serious’’ akajibu Imma ‘’ okey tuachane na hayo mimi naitwa Rose Martini nina mwaka wa pili chuoni hapa nimetokea Tanzania Mkoani Tanga ninachukua Degree ya kwanza ya udaktari sijui mwenzangu’’ alijieleza kwa kujiamini sana mrembo huyu Rose.
   ‘’mimi naitwa Mr: Imma Salim nafurahi kukufahamu sio tu ,kwakuwa mtanzania mwenzangu bali mtanga mwenzangu ninachukua Digrii ya pili biashara  na nina miezi mitatu tu chuoni hapa’’alijieleza Imma.
 Nashukuru  sana kukufahamu au kufahamiana na wewe unjua ni vigumu kukutana na mtu wa nchi mmoja nje yam chi mara nyingi huwa ni bara moja au hata nchi moja anaendelea Rose.
huwa unapendelea kukaa maeneo gani hapa chuoni maana last time nilikuona canteen la leo hapa, aliuliza Rose.
Huwa napenda sana hapa vipi unaishi ndani ya chuo au umepanga nje? aliuliza Imma.
No naishi humu humu chouni mimi maisha ya nje ya chuo nayapenda sana ila Baba hataki hata kusikia.alijibu Rose.
 ok sasa vipi ngoja nikakuchukulie bia alisema Rose huku anaamka.
Hapana kwa kweli sijawahi kunywa bia na sifikirii kama nitakuja kunywa hata siku moja
lakini pia huu ni muda wa mzaoezi naomba nienda tutakutana tena alijibu Imma huku akiamka.
poa ucjali naweza pata namba ya simu maana tumeshakuwa ndugu sasa. anamlizia Rose kwa kuomba namba ya simu pia ningependa unipe ramani, anuani na hata namba ya wazazi wako ili tukifika Tanzania tuwasiliane pia aliomba mrembo Rose kwa jinsi alivyoumbikani wazi kwamba kama akiamua kugombea umiss basi Tanzania tunashinda miss World.
     Kwani kuguo chake kifupi na mapaja yake malaini yalozungukwa na tite nyeupe yakiwa wazi huku akiwa amevaa kishati cjha kubana chenye kuonesha mzaiwa yalochomozea kama nchi ya bamia yakiwa yanaonekana kwa juu na ndani kwani shati lilonesha kila kilichoko ndani.
Mmmmmmhh Imma atafanyajeee endelea jumaapili ijayo hapa kwenye hii blog yetu.
  Unaweza toa maoni yako pia.


SEHEMU YA PILI


Imma alimpatia namba na ramani kama alivyoomba huku akichukuka za kwake kwa nia ya kudumisha mawasiliano kama ndugu.
Kwa muda mfupi tu Imma na Rose waliweza kuzoeana na kupeana faraja kwa kutembelea sehemu tofauti.
Ingawa hii ilimfanaya Imma kujua maovu ya Rose kwani kwa kifupi ni mrembo anaependa sana starehe.
 Weekend ya tatu toka wafahamiane Rose alimuomba waende Night Club’
Rose” can you take me to flash night club please”
Mmmhhh its ok even if am not used to,but I will,don’t worry coz I don’t mean to borther you. Alijibu Imma.
Ilikuwa ni ujumbe mfupi wa simu (sms) kutoka kwa Rose.
siku hiyo usiku Rose alivaa skin jeans nyeupe na t-shirt black huku mguu akiwa na kicheni cha gold,kiunoni alikuwa na cheni ya gold,
T-shirt yake haikuweza kuficha kile kilichopo kiunoni. Huku umbo lake la namba nane na pisto za mapaja kama zinataka kupasua skin jeans huku akiwa anaelekea kwa  Imma.
Imma am out please can we go ilikuwa ni sauti ya mrembo Rose akiita nje pembeni kidogo na moja ya dirisha la nyumba zakuishi wanachuo ambapo imma alikua akiishi, “ok come in am just to finish” ilikuwa sauti ya Imma, baada ya muda Rose alikuwa ndani. Ok nipe kama dakika tano please aliomba imma huku Rose akitingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana na maombi hayo.
Mmmmmmhhhh huyu dada jamani mtihani huu nitafaulu kweli? Alijiuliza imma kama ishara ya kuchanganyikiwa na mavazi na umbo la mrembo Rose usiku huo.
“Ok how do we go” aliuliza Rose, we will use my bike alijibu imma.
Mmmhh no please is not safe why cant we use tax please? alichangia Rose.
No lets use bike its simple,safe and flexible.
Ok we will don’t worry imma alikubali Rsoe.
Alitoa pikpiki aina ya BMW ambayo huitumia kwenye mizunguko ya ke ya hapa na pale mjini, Rose alipanda huku kiuno chake chenye cheni ya gold kikiwa wazi huku umbo lake nikidhihirisha uwezo wa Mwenyezi mungu kwenye uumbaji..
Ilikuwa ni safari ya zaidi ya dakika kumi kwa mwendo wa kawaida sana huku safari yao ikitawaliwa na stori za Tanzania.
“Can you take some bear please”? ni sauti ya Rose muda mfupi baada ya kukaa kwenye kwenye meza iliyoko pembeni kidogo na mwanga ulokuwa ukimulika kwa kufifia na huenda ndo sababu ya kuitwa ukumbi huo flash night club ilioko jiji la Ottawa,eneo la 400 dalhousie kati ya besserer na Rideau nchini canada
 ambao hufunguliwa kila ijumaa na jumamosi tuu,kuanzia saa tatu ucku hadi kumi asubuhi.
“Thanks Rose am not tarking alcohol” huku akiagiza maji.
Baada ya maongezi na muzik wa hapa na pale siku ilionekana kuwa nzuri sana kwa Rose hasa baada ya kupata kilevi,ingawa kwa imma ilionekana ya mawazo sana kwani hakupanga kuwa na msichana akiwa masomoni lakini kwa pozi za Rose mmmhh akili ilianza kubadili mawazo.
“Please I don’t feel like going there my self please lets finish a day” mmmh ilikuwa ni sauti ya Rose huku akiwa amemkubatia Imma kwenye bike (pikipiki) wakati anakatisha kumpeleka kwake kuku wakiwa hoi kwa mziki ni pilika za club
What wwhhat do you mean Rose? Aliuliza Imma.
I mean take me to your place please we have been together from that time please lets close the day with destiny of our happiness. Alikazi Rose huku akionekana kuwa serious kwa kile anachokisema.
Imma alitafakari kwa kina kuhusu ombi lile huku akiamini amefanikiwa kumbeba temba kwenye bajaji,kisha akaona ni heri kwake huku akijawa na uchu wa kumpata mrembo huyo kiulaini
Mmmmhhh please can we go together my best,No please just do it first then I will after, ilikuwa ni malumbano baada ya kufika kwa Imma huku Rose akikataa kuoga peke yake.
Imma inahisi anaua tembo kwa ubua lakini ghafla Rose akiwa bafuni simu yake inaingia sms,ghafla Imma anapata hamu ya kuifungua ghafla anapigwa na butwaa “Sweetie I saw you with African its your time to give others as you gave it to me, but note that you have distructed my life and my strengths are no longer as before, am dying just because of you,good night” ulikuwa ujumbe mfupi ulosaviwa kwa jina la Never.
Its you now, unaju yale maji ni baridi hadi pombe yote imekwisha ilikuwa sauti ya Rose huku Imma akiwa hana raha kwa ujumbe tena muda huu wa usiku.
I dont feel like eating anything am full lets us sleep ni sauti ya imma baada ya Rose kudai ameshiba ila nataka Imma ale,
Alivua taulo taratiiibu na  kupanda kitandani huku mziki ukisikika kwa mbali lakini Imma amejawa na mawazo,mmmmh are you ok imma?
for sure am not may be because of dancing alijibu imma kuku akiwa hayuko tayari kumueleza nini kimetokea.
rose aliishika simu yake na ghafla akaona ile messahe ikiwa imefunguliwa .
aliisoma kwa makini sana kisha huku imma akimuangalia kwa jicho la pembeni ili kuweza kugundua lugha ya sura yake baada ya kuisoma kitu kilichomchanganya zaidi ni kwa Rose kutostushwa na sms ile zaidi ya kuisoma na kuidharau kwa kukunja mdomo kisha akaizima na kuiweka pembeni huku akimtaka Imma amlalie kifuani.
no no no Rose i can live live like this? alifoka ImMa huku akiamka na kukaa kitandani.
kwani ni nini Imma mbona sikuelewi au ni hii sms ya huyu mpuuzi ndo inakuchanganya?
mpuuzi mpuuzi aje weakati jamaa anakufa? alijibu Imma kwa kufoka.
"anakufa ndio si anakufa kwa ujinga na atamaa zake" alijibu Rose huku akigeukia upande wa pili wa kitanda  huku jibu hilo likizidi kumchanganya akili.
tafadhali Rose naomba amka ulieleze kwa upanda unachomaanisha, alianza kuwa mdogo na kuongea kwa sauiti ya chini.
no no no imma nimechoka tafadhali naomba uniache, hebu tulale tutalongea hii mada kesho.
   

Nini kitaendelela je kunalalika na nini kimejificha kwa Rose na Imma anawza nini?
usikose sehemu ya tatu ya hadith hii yenye ukweli ndani yake.
Pia unaweza kutoa mawazo au swali.
Mungu ndo mwangaza wetu kwa kila jambo.




SHEHEMU YA TATU:


No no no Rose i can live live like this? alifoka Imma huku akiamka na kukaa kitandani.

kwani ni nini Imma mbona sikuelewi au ni hii sms ya huyu mpuuzi ndo inakuchanganya?

mpuuzi mpuuzi aje weakati jamaa anakufa? alijibu Imma kwa kufoka.

"anakufa ndio si anakufa kwa ujinga na atamaa zake" alijibu Rose huku akigeukia upande wa pili wa kitanda  huku jibu hilo likizidi kumchanganya akili.

tafadhali Rose naomba amka ulieleze kwa upanda unachomaanisha, alianza kuwa mdogo na kuongea kwa sauiti ya chini.

no no no imma nimechoka tafadhali naomba uniache, hebu tulale tutalongea hii mada kesho.

  

“Hapana naomba uniweke wazi juu ya suala hili” aliendelea kuhoji Imma.

Huyu jamaa anadai ananipenda sana na kamwe hawezi kuishi bila ya mimi ni kijana kutoka Nigeria na nmemeshamwambia kwamba hatuwezi kuwa pamoja, alieleza kwa ukali Rose.

“but you talk hukuwahi kuwa na uhusisanao na ilikuwaje jamaa anakusumbua hivyo na ujasiri gani ulikufanaya kutokuwa nae”?

Try to understand Imma I just don’t need the guy that all, please lets get sleep am  tired.

Ok your wish is my command lets sleep but nothing I can with you this night unless I know the truth.   “Its ok lets sleep I can’t ague with you just because I love you imma”

Imma hakuwa na amani kabisa kiasi cha kukosa hata hamu ya kufanaya tendo na Rose kwani ile sms ilimfanya awaze usiku mzima huku akiamini Rose anasiri kubwa kuhusu yule jamaa.

        Mahusisano yaliendelea ingawa Imma alihakikisha hawaliendei tendo la ndoa.

Ndani ya uhusiano wao Imma aligundua mengi kuhusu Rose ikiwemo tabia yake ya kujichanganya na wadada waloshindikana chuoni hapo huku akitoka na wanaume wa aina tofauti ingawa hakuwahi kukubali hilo mbele ya imma,huenda ni kwa kuwa alimpenda ndo maana aliogopa kumpoteza.

Miezi mine mbele Rose alimaliza mitihani yake ya mwisho na kurudi Tanzania huku akimuacha Imma nchini Canada.

        Akiwa Tanzania Rose aliomba kazi kwenye Hospital iliyoko ndani ya mkoa wake wa Tanga kwani hakupenda kuwa mbali na wazazi wake ambao aliwamisi kwa miaka kadhaa.

akapata kazi kwenye hospital ya Bombo mkoani hapo akiwa anamawasiliana na Imma kupitia kwenye email na simu,huku akiendelea kumuomba avumilie kwa kumhakikishia kuwa yeye yuku Tanzania na hawezi kuwa na mtu hadi yeye atakaporudi.

Mkaisha ya Rose jijni Tangu aylikuwa mazuri kwani alikuwa akilipwa vizuri achana na ukweli kwamba familia yake ilikuwa ikijiweza kiuchumi.

Alijitahihdi kudumisha mawasiliano na Imma hadi Imma alipohitimu masomo yake..

          Baada ya mwaka mmoja na nusu Imma alikuwa ameshamaliza masomo yake nchini Canada na sasa inabidi arudi nchini Tanzania, mapokezui ya Imma yalifanywa kwa siri sana na Rose kwani alitoka tanga na usafiri binafsi na kumfuata Imma jiji dar kisha akampeleka hoteli maeneo ya magomeni mapipa ijilikanayo kwa jina la  New Bondeni hoteli,kitu kilichomshangaza Imma ni pale Rose alipomkataza hata kuonana na Rafiki yake wa karibu Iqram Imamu  ambae baada ya kuhitimu wote chuo cha elimu ya bishara (cbe) alianzia ofisi inayojihusisha na ajira za walimu hapa Tanzania Teaches’ Junction iliyoko maeneo ya hapo hapo magomeni huku akidai kwamnba amechoka hivyo anapaswa kupumzika, asubuhi alimchukua na kumpeleka moja kwa moja Tanga.

 Wakiwa tanga walikuwa karibu kaka marafiki wa wakaida.

Baadaa ya miezi mine kupita Imma huku akifanya jitihada za kutafuta ajira kwenye maofisi mbalimbali mwishowe alifanikiwa kupata kwenye kampuni  kusafirisha mbao nchi za nje iliyoko mkoani Tanga Costal Forest Trade akawa anafanya kazi kama meneja wa usafirishaji kwenye kampuni hiyo.

  Baada Mwaka mmoja kazini hapo huku kila mara rose anakuja nyumbani kwao na wakati mwingine walikwenda wote Club Lacasa kujirusha lakini Imma alijitahidi sana kumshawishi Rose ampe ukweli wa ile sms  lakin Rose alishikilia msimamo wake kwamba yule kaka alikuwa akimtaka nae hakuwa tayari, ingawa imma aliamini kuwa huenda Rose ni Muathirika wa virusi vya ukimwi kwa tabia zake na ile meseji vilimpa picha tofauti hivyo kuamua kiume kwamba hawawezi kuwa wapenzi hata siku moja.. Mwaka mmoja baadae wazazi wa Imma wanamgusia mtoto wao kuoa na kumwambia kwamba itabidi aishi na mkewe hapo hapo kwao ingawaje swala la kuoa kwake haikuwa tatizo kwani alikuwa akilipwa mshahara mzuri tu kwenye kampuni hiyo na kumsisitiza kwamba ni vyema kama anamtu anethani anafaa amlete nyumbani.

     “ni muda sasa umepiata Imma mwanangu sijui una mawazo gain juu ya sula ya kuoa?” ilikuwa ni kauli ya Baba yake mzazi.huku mama akiwekea mkazo,huu ulikuwa muda mchache tu baada ya chakula cha usiku.“Tena kwakuwa  mmeshaguana ni vyema tumite tuu mzee martini tujue nhini kinafuata”

Mmmhhh mama? Imma alishangazwa sana na kauli ile huku akipata picah kuwa wazazi waliamini  kuwa wao ni wapenzi , huku wakiteka amuoe mototo wa tajiri mwenzao ili waishi maisha ya kifme baada ya kusikia taarifa hizo Imma anakataa kata kata na kudai Rose ni rafiki yake na kamwe hawezi kuwa mkewe, ila kwa upande wa wazazi hakuweza kumuelewa hukuwa wakidai kwamba tabia yake inaridhisha kwani hakuwahi kusikia tabia mbaya yoyote hapa jiji kabla na baada ya kwenda chuo na hata baada ya kurudi.

No imma don’t disappoint our family,sikotayari umuoe mwanamke mwingine yoyte mbali na Rose tafadhali mwanagu. Hii ilikuwa kauli ya mama yake imma.

“Mom but she is not my ideal?  How will I marry whom I am not in love with”?

Alihoji imma kwa sauti ya mshangao,

 “Lsten to your mom imma we have discussed these things before here and all what you have as an obstacles we thought about before telling you, so please get ready for Mr.Martin Daughter I real respect my friend I will never disappoint him, this is my last say to you” aliongea maneno hayo makali hkukakiamka na kwenda ndani huyo alikuwa mzee mwanjala ambae pia alifahaika Tanga kwa misimamo ya kauli zake.

  Ilikuwani kauli nzito sana ilomfanya imma kukosa jibu huku akiwa amepewa siku mbili kutoa msimamo wake juu ya kumuoa binti huyo.

  “ Am not happy with  my life anymore,I cant disappoint my parents but I cant live with Rose I don’t love her at all,how will i live with her”ilikuwa ni kauli ya imma akimueleza james ambao walikuwa wakifanya kazi ofisi moja.

  Ok my lovely parents I real respecting you but ………………………….

Endelea kufuatilia hadithi wiki ijayo kwenye sehemu ya nne.

Nini kiatokea na nini penzi la kipofuuuuuuuuuuu

Unaweza pia kutoa maoni yako kwenye hapo hapo kwenye comment.
mungu ndo mwanga wa maisha yetu. 



     SEHEMU YA NNE


Kwa kuwa wazazi walilazimisha imma hakuona sababu ya kuendelea kuwapinga wazazi wake ingawa kwa upande wake hakuwa tayari kwani historia ya Rose alikuwa akiifahamu kabla.
“Ok mum as I told you I will but mind you this is not my decision, I gave you answer but you just think twice about this,getting married is my right and whom to marry is my right too”.
Alitoa jibu hilo kwa sauti ya ukali huku Baba ayake na Mama wake wakibaki wakitazamana kama kutoamini kile kinachotoka kwenye kinywa cha mtoto wao kipenzi.
 swala la kuoa kwake halikuwa tatizo kwani alikuwa akilipwa mshahara mzuri tu kwenye kampuni hiyo tatizo ni kwanin walitaka lazima amuoe Rose mtoto wa tajiri mwenzao ili waishi maisha ya kitajiri wakati yeye anaamini hata bila ya kufanya hivyo tayari angeweza kuishi maisha mazuri tena kwa msichana ampendae
  Shikamoo mzee’’ anasalimia Imma huku akiwaza kuhusu ujio wa wgeni wale,ulikuwa ni msafara wa wazee wapatao ishirini ambao kwa hali ya kawaida walionekana kuwa na hadhi ya juu ingawa imma alifanikiwa kumuona mmoja tu wakati anafungua mlango wa chumbani kwake akitokea store ya magari, akiwa kwenye mawazo “kaka imma,kaka imma” ilikuwa ni sauti ya mfanyakazi wa ndani ikimjuza kuwa alikuwa akiitwa na mzee sebuleni, hapo hofu inaanza kumjia, “ina maana wameshindwa kabisa kufikiria juu ya ukati;I huu ok but I cant marry Rose”yalikuwa mawazo ya imma yakijirudia kichwani mwake baada ya kuitwa.
 ‘’Imma natumai unamfahamu huyu binti na huyu ni Baba yake anaitwa Mzee Martini Hizza na hawa wengine ni ndugu zako utawafamu taratibu lengo la kuja hapa ni kuhusu uchumba na harusi kati yako na Binti yao Rose hivyo naomba uiwasalimu ili tuweze kuendelea ’’alimaliza mzee Mwanjala baada ya maneno hayo mrembo Rose alitoa tabasamu la hali ya juu lakini kwa upande wa Imma hakuonyesha kufurahi bali kujikuta akitetemeka kama mwanaume anaetaka kuozwa ndoa ya mkeka kwani Rose hakuwa chaguo lake.”hatuoni sababu ya kuchanganya familia tusizo zifahamu unajua familia nyingine ni matatizo unaweza kuoza binti ukashangaa mali zako zote zinatoweka” yalikuwa maneno ya mzee Martin,
Ok unaweza kwenda na huyu binti pia kwani hafuatayo hapa hayawahusu baada ya kusiskia maneno hayo aliamka nakwenda moja kwa moja hadi chumbani kwake na kujifungia hiyo ilikuwa ni kauli yam zee mwanjala mzee anaesifika kwa misimamo ya kizamani.
 Baada ya kikao hicho sasa Imma na Rose walikuwa wachumba,kila siku wakawa wanakutana na kuzungumzia maisha yao wakiwa kama mke na mume watarajiwa wakiwa wameshapanga ahadi ya harusi yao je.
 Imgawa kwa upande wa imma hakuwa akiifurahia ndoa hiyo huku akiwaza kutoroka nyumbani wazo ambalo huvurugiga tu baada ya kumkumbuka mama yake kipenzi Salama hivyo kujikuta akiingia kwenye maamuzi pasi na kuridhia.
Mwezi mmoja kabla ya harusi ya kitajiri kila kitu kilikuwa tayari na kila pande ya jij hilo la Tanga ilikuwa na taarifa juu ya harusi hiyo ambayo inasubiriwa kwa hamu na wakazi wa Tanga ili kuona nin kitafanyika kwani mzee martini aliahidi kushanga jiji hilo kwenye harusi ya binti yake kipenzi.

   Imma akiwa ndani ya gari yake ya  kazini aina ya Rava 4  kwenye makutano ya barabara za kisosora na stendi kuu ya jiji hilo lilobarkikiwa kwa viwanda na kilimo.
               Ni majira ya saa kumi na moja joini akiwa amechoka kwa kazi za siku nzima huku kichwa chake kikitawaliwa na mawazo mfano wa mama alopoteza mume,nyumba,kazi na watoto kwa wakati mmoja  akiwa anatoka kazini kuelekea nyumbani anajikuta kifunga breki za gafla baada ya msichana mmoja kupita karibu na gari huku akiwa speedi ya stini anafunga breki ya ghafla huku akijikuta akitekemeka mara anashuka huku akiwa ametawaliwa na hasira kali kwa lengo la kumpiga huku akiwa anafoka ‘’mmpumbavu mkubwa kwanini Unataka kunisababishia ajali ina maana hunioni na hata ungurumo wa gari huusikii au ndio mnataka madereva tuwapishe ninyi?’’ilifoka kwa hasira kuhu akiwa amepaki vibaya na kusababisha  foleni ya magari yapatayo thelathini .
 ‘’ naomba unisamehe kaka mimi sioni na wala wala sio kosa lako naomba nisamehe kaka’’ ni sauti ya msichana akiwa ameshika fimbo alioashiria kuwa ni mlemavu wa macho (kipofu) akiomba msamaha huku akilia kwa uchungu huku akikimbia kando ya barabara huku akipapasa papasa na kifimbo hicho.
     Imma alishusha pumzi na kumuomba msamaha yeye ‘’sikufahamu dada naomba nisamehe kwa kukufokea, imma alirudi kwenye gari na kupaki vizuri ili magari mengine yapite kasha akarudi kwa yule binti ambae alikuwa pembeni akilia huku akitetemeka “binti naomba unisamehe tafadhali najua unavyojisikia tafadhali sikuwa nafahamu hali yake naomba twende kwenye gari nikupeleke unakoelekea tafadhali’’ sio siri Imma alimuonea huruma sana  ‘’samahani kaka nisikupotezee muda nashukuru kwa kunisamehe kwani huenda unge sababisha ajali na kuharibu maisha yako pia nashukuru kwa roho yako ya huruma ila naomba uende tu ‘’ Imma alitamani kulia nakujutia hasira zake na wala hakuwa tayari kumuachia  alimbembeleza lakini hakuwa tayari kupanda kwenye gari huku akiomba imma amruhusu aende nyumbani kwani yeye ndo mwenye funguo.
“ingawa huko tayari kuniruhusu nikupeke basi hata jina lako na wapi unaishi tafadhali”
Hapana kaka tafadhali naomba usinidhuru tena sina sabau ya kukupa jina langu wala wapi na kaa tafadhali naoma niache niondeke alisema binti.
Wakati imma akiwa amemshika mkono akimbembeleza asilie kwa mbali anaona gari ya Rose ikwa inakuja kwa speed kali kuelekea aliko imma.
    Mmmmmmmhhh nin kitafuatia yule Rose anakuja kufanya nin na kwanin yuko speedi kiasi hicho……………………………………..??????.
       
         usikose sehemu ya tano ya hadithi hii yenye ukweli ndani yake. 
 Unaweza pia kutoa maoni yako kwenye hapo hapo kwenye comment.
                       “mungu ndio mwanga wa maisha yetu”





SEHEMU YA TANO

Hapana kaka tafadhali naomba usinidhuru tena sina sabau ya kukupa jina langu wala wapi na kaa tafadhali naoma niache niondeke alisema binti.
Wakati imma akiwa amemshika mkono akimbembeleza asilie kwa mbali anaona gari ya Rose ikwa inakuja kwa speed kali kuelekea aliko imma.
Mara imma akastuka kuona gari ya Rose ikiwa speed kuelekea walipo, ila ghafla gari ile iliwapita kwa speed ile ile ndipo imma aligundua kuwa aliekuwa akiendesha hakuwa Rose bali ni mdogo wake anaitwa Innocent ingawa pia aliwaza kuwa ni kwanini alikuwa speed kwa kiasi hicho.
Tafadhali kaka unanichelesha nyumbani, mimi naitwa salma Ramadhani ninaishi barabara ya kumi nane ni mwalimu wa watoto wasioona akaishia hapo ‘’nashukuru kwa kuridhika tufahamiane  mimi naitwa Imma salimu ni meneja kwenye kampuni kusafirisha magogo nje ya nchi’’alijieleza kwa ufupi  kijana Imma ila akawa hajaridhishwa na  maelezo ya salma ikambidi amuombe wakae sehemu ili waongee Salma  alikataa kata kata kwa madai kuwa anachelewa kurudi nyumbani Imma alijitaidi ata kumuomba ampeleke kwake kwa gari yake lakini Salma hakuwa tayari, ‘’basi naomba japo namba yako ya ’basi naomba japo namba yako ya simu Salma mbona unakuwa hivyo kumbuka binadamu hufahamiana kwa namna tofauti amini hii ndio njia pekee aloweza kutukutanisha mwenyezimungu’’ alilalamika Imma ila Salma alimjibu kuwa hana mawasiliano mengine zaidi ya kumueleza anapoishi ikamlazimu  Imma kuridhika na maelezo ya salma akaingia kwenye gari na kurudi nyumbani huku akitamani sana kwenda kukutana na Salma kitu ambacho aliamini kinawezekana ingawa hata ramani aliopewa isingemuwezesha kufika akaendelea na safari ya kuelekea kwake huku akiwa na mawazo mengi juu ya salma Ramadhani.msichana huku akitamani sna kujua miasha yake na hali ile inatembea barabarani bila hata msaidizi “mmmhh yule dada itakuwa anaishi na nani maskini ya mungu mmmmhh lakini Salma ni mrembo kwani mungu angempa macho kweli ingekuwa balaa’ aliwaza Imma akiwa amejitupa kwenye coach la chumbani kwake.
Salma alikuwa akiishi na dada yake tu ambae hakuwa na baba wala mama kwani wote walifariki kwenye ajali gari iliyotokea iliyoluwa ikivuka kwenye pantone ya kivukoni kwenda posta na kupoteza maisha hapo hapo wakiwa na kaka yao na mdogo wao wa kike (mwanahuba) ambapo walikuwa wakimsindikiza Mwanahuba shuleni Ruvu  miaka sita iliyipita  na kwa kipindi chote hicho alikuwa akiishi na dada yake ambae ni mwalimu wa shule ya msingi kisosora na muda huo alikuwa anamfuata dada yake ambapo ni kawaida yake baada yeye kutoka kazini kumfuata dada yake ambae anafanya karibu kidogo na kazini kwake na huwa wanarudi wote, ila hakupenda kumruhusu mwanaume amchezee mwili wake hata mara moja kwani alikuwa akihusiwa na dada yake kila siku huku ukizingatia kuwa baada ya Wazai wao kufariki hawakuweza kusomeshwa zaidi ya dada yake huyo alouza badhi ya mali na kujiunga na chuo cha ualimu wa shule ya msingi na kupangiwa kisosoro mjini Tanga  kizingatia kuwa yeye ni kipofu alifahamu kuwa hakuna mwanaume ambae angekuwa mkweli zaidi ya kumchezea na kisha kumtupa hivyo aliapa kutompa mwanaume yoyete nafasi hata ya kusumbua ubongo wake.
Imma aliendelea kuumiza kichwa juu ya maisha ya Salma baada ya siku kadhaa akiwa anahangaika na picha ya Sama ambayo haitoki kichwani mwake akiwa amepunguza baada ya kazi akiw na rafiki yake kipenzi James Mhina, Imma akajikuta akimsimulia kile kilichomtokea sikuchache zilkizopita huku akionesha kuguswa kwake na tukio hilo, ingawa ilikuwa tofauti na matarajo yake kwani kwa upande wa james mambo yanakuwa tofauti na alivyotarjia Imma ‘’my best unachekesha yaaani unaumiza kichwa juu ya binti usomfahamu,kibaya zaidi ni  kipofu na wakati unatakiwa kunipa habari za mkeo mtarajiwa Rose sasa kipofu maisha haya ni nin kama sio mikosi na matatizo ya maisha, fikiria Rose mtoto mwenye mvuto halafu humtaki sasa utaishi nae vipi?hicho kitakuwa kituko’’alimaliza kwa kuponda na kumfanya Imma amuone James kuwa  ni adui wa mawazo alikuwa nayo.
 ‘’Yani best unadiriki kunitamkia maneno hayo sawa tufanye yameisha’’alilalamika Imma na kuishia kwa neNO yameisha kwani hakuwa muongeaji sana ila roho ilimuuma sana. Kwani alikjikuta hana mtu wa kuweza kumuelezea hisia zake za ndani na namna gani lile swala limemgusa.
Kesho yake mida ya saa tano mchana aliamua kwenda kumtafuta Salma huku kiwaza  ‘’kwa kuwa leo ni jumamosi natumai nitamkuta nimueleze yaliyo moyoni mwangu’’ baada ya mwendo wa dakika ishirini ndani ya Rava 4  anawasili barabara ya kumi na na nane akiwa hajui amuulize nani anaamua kushuka na kumuita kijana mmoja aliyekuwa nje ya nyumba nyumba moja mbovu mbovu’’samahani namuulizia dada mmoja anaitwa Salma  Ramadhani “mmmhh hapana hapa mtaani hakuna dada mwenye jina hilo” alijibu yule kijana jibu ambalo lilivunja matumaini ndani ya ubongo wake,ghafla alimuona mama mtu mzima akikaribia walipo “samahani mama anmuulizia dada mmoja hapa mtaani anaitwa salma  nimlemavu wa machohuwa anatembelea na fimbo sijui unamfahamu ‘’ Yule mama alikaa kwa muda kidogo akiwaza kisha ‘’hao wadada wapo wawili hapa mtaani ila majina yao siwafamu mmoja ni mwalimu mwengine anasoma sijui unamuulizia yupi? ‘’alimaliza Yule mama baada ya kusikia hivyo Imma alianza kuonyesha tabasamu na akijikuta akijibu kwa pupa’’ huyo ambae ni mwalimu’’yule mama alimuelekeza kuanzia pale kwenye nyumba nyeupe hesabia nyumba ya kwanza , ya pili ya tatu ndio yao ahsante sana kijana chukua hii pesa na mama hii  itakusaidia alitoa noti shilingi alfu  tano na alfu kumi na kuwapa ‘’jamani ahsanteni ‘kisha Imma akaondoka kuelekea alipoelekezwa  ‘’hodi’’ aligonga mlango mara akasikia sauti ikimuamuru aingie.
  Ilikuwa ni nyumba moja ambayo ilionekana kuwa ni ya zamani ambayo kwamba hata mtoto anaweza kugundua kuwa ilikuweko kabla ya Tanganyika haijapata uhuru, Imma aliingia ndani na kumkuta dada mmoja ambae hakumfahamu ila alionekana kuwa ni mtu mzima kidogo ‘’Shikamoo dada  aliamkia Imma ‘’
‘’marahaba kijana  unashida gani?aliuliza  Yule dada
  ‘’samahani dada mimi naitwa Imma nilikuwa namuulizia dada mmoja anaitwa Salma Ramadhani nimeelekezwa hapa sasa sijui nimemkuta?’’alimaliza kwa kuuliza swali
  ‘’Salma? alishtuka Yule dada baada yakusikia kwa mara ya kwanza mwanaume anamuulizia ila akaona asiendelee kumuhji ila amuite tu Salma na baadae afahamu kitakacho fuata,
 ‘’ndio umemkuta je ukimuona utaweza kumfahamu?
 ‘’bila shaka kwani namfahamu vizuri zaidi,
Yule dada akaingia ndani mara Salma alitoka huku akiwa na wasiwasi mkubwa kwani hakutarajia kitu kama hicho wewe ni nani unaniulizia na je unashida gani na mimi?’’
mimi ni Imma Salimu’’alijitambulisha kwa Salma lakini Salma hakuonyesha kumfahamu ‘’mbona sikufahamu unasema unaitwa Imma?’’aliuliza swali kwa mshangao huku dada yake akiwa anamskiliza kwa makini zaidi,ila Imma hakupenda kuona ile hali ya kutofahamiana na mtu ambae anapenda kuwa na mahusiano nae ya karibu ,akatulia kwa mda kisha akaendelea  ‘’mimi ni Yule dereva uliyekutana nae makutano ya barabara za kisosora na stendi juzi kabla hajamaliza Salma alionyesha kumkumbuka  ‘’ahaa ‘’sasa nimekumbuka haa yani umekuja kwetu unashida gani?aliuliza swali huku kwa mbali akionyenya tabasamu  ‘’usiwe na wasiwasi nimekuja naomba unipatie nafasi tutoke tukaongee Salma samahani kama nitakuwa nimekosea’’alitupa ombi hilo huku akisubirikwa Salma aongee
 we kaka kwanini unakuwa sio muelewa nimekwambia siko tayari kufanya chochote na wewe naomba naomba niache ‘’ alieleza kwa jazba kidogo kiasi cha kumfanya Imma aanze kuchanganyikiwa  ‘’Salma naomba usiongee maneno hayo naomba nielewe Salma kasha unisikilize.
 ‘’nimeshakwambia siwezi kwenda na mwanaume yoyote huo ndio  ukweli wangu samahani  kama nitakuwa nimekosea’’dada yake alimdakia ‘’we Salma naomba uende nae msikilize huyo ni mwenzio hujui anataka kukwambia nin?alimaliza kwa maneno hayo na kumfanya Salma aanze kutafakari na kujikuta akiitikia ‘’sasa dada’’ ‘’sasa nini unakosa ustarabu’’baada ya mazungumzo hayo Salma alienda ndani huku akiwaacha dada na Imma wakiwa wameduwa wasielewe aidha amekubali au laa,baada ya kimya cha dakika kama saba Salma alitoka akiwa amependeza kiasi cha kumfanya dada yake aanze kumtania
 ‘’he Salma hiyo safari ulikuwa umeshaipanga nini?’’ila Salma hakjibu kitu alikuwa akiendelea kupapasa njia ya kutokea na kumfanya Imma asielewe kama wanakweda au anasafari zake  ‘’twende”,.Dada tutakutana baadae kama nitarudi salama’’aliamrisha huku akiambatanisha na kuaga.
 Imma alimfuata na kumshika mkono hadi kwenye gari lake wakaingia na kuanza safari kuelekea hotel ya MK. INN ambayo ni maarufu sana jiji hapo .
Wakiwa wanakaribia MK Hotel Imma anashangaa kuiona gari ya Mzee Martin akiwa anawaza atafanyaje kama mzee martini baba mkwe wake mtarajiwa atakuwa pale nin kitafuata? mara kwa pembeni anaiona gari ya Rsoe ndipo akagundua familia kuwa Familia ya Mzee martini ilikuwa hapo ikiwa ni Rose,Mama yake na Baba yake.
Mmmmmhhhhhhhhhhh hayaaaaaa usikose sehemu ya sita

If you can't accept your wrongness you can't determine your weakness
“mungu ndio mwanga wa maisha yetu”







Sunday, 26 May 2013




TANZANIA IDEAS CENTRE TANZANIA  (TIC)

TEACHERS’ JUNCTION
        Teachers’ Junction Organization inyojihusisha na ajira za walimu nchini.
Tunashukuru kwa mchango wetu ambao mmeunesha tangu kuazishwa kwake hadi hapa ilipofikia.
Kwa sasa tunawaarifu vijana wote Tanzania na nchi jirani hususani wana jamii forum kwamba tunaanzisha TANZANIA IDEAS CENTRE (TIC).
Ambapo vijana kutoka sehemu tofauti Tanzania na nchi jirani tutakutana na kuunganisha mawazo ya kibiashara na namna ya kuziazisha yenye lengo la kuunganisha vitu watatu muhimu kwenye biashara:-
1)      WAZO LA BIASHARA
2)      UWEZESHAJI
3)      MTAJI

TANZANIA IDEAS CENTRE
Tunahiji  Vjiana 30 kuunda uongozi wa TIC na kujadili malengo yaliyopo na walionayo.
TIC inarajia kuanza kufanya kazi rasmi mwanzoni mwa mwezi wa Saba mwaka huu.2013.
Kwa walio tayari kujiunga na TIC sifa :
·        Awe kijana wa kiafrika
·        Elimu kuaznia kidato cha nne na kuendelea
·        Umri kuanzia miaka 25 hadi 40.
·        Mwenye mawazo pevu na busara

 Mawasiliano:
TIC organizer
Mr. Njama
Phone:  0783-810857
    Unaweza ku-like page yetu na kucha maoni yako.

Thibisha ushiriki wako kwa kutuma email na Cv zako kisha utajaza form za kujiunga.
Wote watakao thibisha kushiriki watashiriki kuchagua uongozi wa TIC.
Taarifa zote zitapatikana hapa hapa jamii forum.

                 HAKUNA MALI[PO KWENYE KUJIUNGA NA TIC

              VIJANA TUKIUNGANA TUNAWEZA KUTOKOMEZA TATIZO LA AJIRA
                           TANZANIA NA AFRIKA KWA UJUMLA
                                                        “With TIC we can Change”